Muda wa kazi: Mon - Fri 8.00 am - 5.00 pm

MAMLAKA YA MAPATO ZANZIBAR

"Tulipe Kodi kwa Maendeleo ya Zanzibar"

ZRA Yakabidhiwa Kombe la Zanzibar Heroes

ZRA Yakabidhiwa Kombe la Zanzibar Heroes

Na. Muandishi Wetu.

Mamlaka ya Mapato Zanzibar (ZRA) imeahidi kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali katika Sekta mbali mbali ikiwemo ustawi wa Sekta ya Michezo nchini hasa Mpira wa Miguu.

Ahadi hiyo ilitolewa jana na Kaimu Kamishna Mkuu wa ZRA ndugu Said Ali Mohamed katika ofisi za ZRA Mazizini wakati wa hafla ya kupokea Shukrani kutoka kwa Shiririkisho la Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFF) kufuatia udhamini wa Timu ya Taifa ya Zanzibar (Zanzibar Heroes) katika mashindano ya Mapibduzi Cup yaliyofanyika mapema mwaka huu.

Akizungumza wakati wa kupokea shukurani hizo zilizoambatana na kukabidhiwa Kombe la Mapinduzi Cup, Kamishna Said alisema Serikali imekuwa ikifanya jitihada ya kuimarisha miundomboinu ya michezo hivyo kuna haja kwa ZFF kupanga mikakati imara ili iendelee kusifika katika mchezo wa Mpira wa miguu.

Katika hatua nyengine ZFF imelezwa kuwa bado ina kazi ya kuhakikisha inaibua vipaji vya vijana katika mchezo wa mpira wa miguu ili kuendana na dhamira ya Serikali ya Awamu ya nane ya kujenga Vituo vya kuibua Vipaji (Footbal Academy).

Sambamba na hayo Kamishna Said alisema kitendo kilichofanyika hivi karibuni katika mashindano ya Mapinduzi Cup Dunia imelewa na kuona vipaji vilivyopo Zanzibar hivyo ni vyema vipaji hivyo vikaendelezwa huku ZFF ikiendelea kubuni mipango thabiti ya kuibua vipaji vyengine visiwani Zanzibar.

Aidha aliwapongeza wachezaji na viongozi wa Zanzibar Heroes kwa kiwango kikubwa walichokionesha katika mashindano ya ”Mapinduzi Cup 2025” na kumuheshimisha Rais wa Zanzinbar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi pamoja na Wazanzibari na Watanzania kwa ujumla.

Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Fedha na Mipago wa Shirikisho la Mpira Zanzibar (ZFF) Ndg. Awadh Maulid Mwita, aliipongeza ZRA kwa kuwaunga mkono na kuwapa mashirikiano makubwa wakati wa maandalizi ya Mashindano ya Mapinduzi Cup kwa mwaka 2025.

Hivyo, Uongozi wa ZFF umeahidi kuendelea kuwa mabalozi wazuri katika kutoa elimu ya ulipaji kodi wa hiari ili kuona Wafanyabiashara na wananchi wanawajibika katika jambo hilo kwa Maslahi mapana ya Zanzibar.

Papo hapo ameiomba Mamlaka ya Mapato Zanzibar (ZRA) kuendelea kuwaunga mkono ZFF pale wanapokuwa na uhitaji katika usimamizi wa aendeleo ya Mpira wa Miguu.

Kwa upande wake Mratibu wa timu ya Zanzibar Heroes Ndg. Hassan Mussa Ibrahim, aliahidi timu hiyo itaendelea kufanya vizuri katika kila mashindano itakayoshiriki na kuendelea kuiweka Zanzibar katika ramani ya dunia kimichezo.

Previous Wataalamu wa Kodi Afrika Mashariki Wakutana Zanzibar

Leave Your Comment

"Tulipe Kodi kwa Maendeleo ya Zanzibar"

Ramani

Contact Details

P. O, BOX 2072, Mazizini- Zanzibar
Opening Hours:
Mon – Fri: 8:00 am – 5:00 pm

ZRA News & Updates

The latest ZRA news, articles, and resources, sent straight to your inbox every month.

Zanzibar Revenue Authority - © 2025. All Rights Reserved

“Tulipe Kodi kwa Maendeleo ya Zanzibar”

0